KAMPUNI ya Ngano Azania imekabidhi jezi seti nne kwa timu ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa FC), Baraza la Wawakilishi, Tanzania Stars na timu ya Zanzibar Veterani kwa madhumuni ya kutumika katika mechi maalum za kusheherekea sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Jezi hizo zilikabidhiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Kampuni ya Adhania, Bw. Awadh Fuad na Meneja Masoko wa Kampuni ya Ngano ya Azania, Mohamed Bashrahil katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa Hadees.